Mwanamuziki kutoka nchini Marekani Rihanna anaelekea mwaka wa sita bila kuachia kazi yoyote ya muziki lakini kila siku anaweka rekodi.
Rihanna ameandika rekodi nyingine kwa video yake “stay” kufikisha jumla ya views bilioni 1 kwenye mtandao wa youtube.
Hii inamfanya rihanna kutanua rekodi yake ya kuwa msanii wa kike mwenye video nyingi zaidi zenye watazamaji zaidi ya bilioni kwenye mtandao wa youtube,kwani amefikisha jumla ya video 8 za muziki.