You are currently viewing RINGTONE APOKO ATAJA KIASI CHA PESA ANAZOLIPISHA KWENYE SHOWS ZAKE

RINGTONE APOKO ATAJA KIASI CHA PESA ANAZOLIPISHA KWENYE SHOWS ZAKE

Msanii asiyeishiwa na matukio kila leo Ringtone ameamua kutaja kiasi cha pesa anacholipisha kwa show zake  iwapo utahitaji kufanya kazi nae.

Katika mahojiano yake hivi karibuni Ringtonr ametangaza kuwa analipisha kwa show moja shillingi millioni 1 na shilling million 1.5 za Kenya kutokea kwenye klabu (Club Appearance).

Ringtone ambaye juzi kati alitangaza kujiunga na muziki wa kidunia amesema amechukua hatua hiyo kutokana na mapromota kumhitaji sana  kwenye shughuli zao kwani amekuwa akitoa muziki mzuri.

Lakini pia ametangaza kubadilisha jina lake la usanii kutoka kwa Ringtone kwenda kwa Blingtone huku akiri kuwa mapato ya nyimbo zake za Injili ambazo aliziimba kipindi cha nyuma itaenda kwa watoto mayatima.

Ringtone amedokeza ujio wa ngoma yake mpya ambayo itaingia sokoni wiki hii ikiwa ni siku chache zimepita tangu atangaze kuanza kuimba nyimbo za mapenzi.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke