You are currently viewing RINGTONE ASHUTUMIWA KWA KUVAA SAA FEKI AINA YA RICHARD MILLIE

RINGTONE ASHUTUMIWA KWA KUVAA SAA FEKI AINA YA RICHARD MILLIE

Miongoni mwa mijadala mikubwa kwenye kiwanda cha burudani nchini ni saa ya bei ghali aliyonunua Ringtone aina ya Richard Millie mwishoni mwaka wa 2021 aliyodai kuwa ameinunua kwa shilingi milioni 47 za Kenya na kusema kuwa yeye ndiye msanii pekee nchini anayemiliki saa hiyo.

Taarifa ikufikie kwamba, ishu hiyo imezua tafrani ya aina yake kwenye mitandao ya kijamii baada ya Kurasa moja mtandaoni maarufu kama Fake Watch Busta kuchapisha taarifa  kuwa msanii huyo alikuwa amevaa saa feki.

Kulingana na Fake Watch Busta saa ya Ringtone imekosa baadhi ya nakshi zinazopatikana kwenye saa Original ya Richard Millie.

Hata hivyo suala hilo limeibua hisia mseto miongoni mwa watumiaji wa mitandao ya kijamii wengi wakihoji kuwa walikuwa wanafahamu saa hiyo ni batili ikizingatiwa kuwa  Ringtone amekuwa akiishi maisha ya kuigiza.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke