You are currently viewing RONALDO AMEVURUGA KIWANGO CHA BRUNO FERNANDES MAN UNITED
RO

RONALDO AMEVURUGA KIWANGO CHA BRUNO FERNANDES MAN UNITED

Cristiano Ronaldo kurejea ndani ya Manchester United kumesababisha mshambuliaji wa timu hiyo, Bruno Fernandes kupoteza ubora wake.

Hayo ni maoni ya nguli wa timu hiyo, Andy Cole ambaye ameeleza kuwa Wareno hao wanapata shida kucheza pamoja.

Fernandes alikuwa staa wa timu na kuonyesha ubora wa juu lakini ameshindwa kuwa katika ubora wa juu msimu huu.

“Kila kitu kimebadilika, Bruno hajawa yule alivyokuwa, ni kama ana hofu ya Ronaldo, nafikiri hatakiwi kuwa na hofu kwa kuwa wote ni wachezaji wakubwa,” alisema Cole.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke