You are currently viewing Rosa Ree kuachia album yake mpya mwishoni mwa mwezi Novemba

Rosa Ree kuachia album yake mpya mwishoni mwa mwezi Novemba

Rapa wa kike kutoka Tanzania Rosa Ree ametangaza rasmi ujio wa album yake mpya iitwayo “Goddess” ambayo ameitaja kuiandaa kwa takribani miaka minne.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram amebainisha kwamba, anaachia album yake hiyo kama msanii anayejitegemea mwenyewe yani adhaminiwi na lebo yoyote na wala hajauza muziki wake kwa kampuni yoyote ya usambazaji wa muziki.

Hitmaker huyo wa “Watatubu” amesema kampuni nyingi zilimfuata kutaka kumdhamini lakini amesema amechagua kumiliki muziki wake kwa asilimia mia.

Hata hivyo ameeleza kuwa albamu yake hiyo itaingia sokoni Novemba 26 mwaka huu,  huku akisema album ya Goddess ina aina mbalimbali za muziki ambazo zinamtambulisha yeye ni nani hasa.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke