You are currently viewing ROSE REE AFUNGUKA KUSAINIWA NA RICK ROSS

ROSE REE AFUNGUKA KUSAINIWA NA RICK ROSS

Msanii wa muziki Bongofleva, Rosa Ree amefunguka kuhusu kusainiwa kwenye lebo ya Rick Ross, Maybach Music Group.

Akizungumza na XXL ya Clouds FM, Rosa Ree amesema anafurahia kuona Rick Ross kakubali muziki wake na mambo yatakapokuwa tayari mashabiki wake tafahamu.

“Kiukweli nashukuru kuona Rick Ross mtu ambaye nimekuwa nikimsikiliza tangia nipo shule anakuwa anakubali kitu ambacho nakifanya, hata nilipotoa wimbo wangu wa mwisho, Blueprint alitoa maoni kwamba ni kitu kizuri”.

“Mambo ni mazuri kwa sababu tunawasiliana, tunaongea na huwezi kujua yajayo yanaweza kuwa ni makubwa sana, sitaki kufichua chochote napenda mfahamu ni kitu gani kitakuwepo huko mbele pindi tutakapokuwa tayari” alisema Rosa Ree.

Ikumbukwe toka ameanza muziki Rosa Ree amepita kwenye lebo kama The Industry na Dimo Production ya Afrika Kusini.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke