You are currently viewing Savara wa Sauti Sol atangazwa balozi mpya wa kinywaji cha Kenya Cane

Savara wa Sauti Sol atangazwa balozi mpya wa kinywaji cha Kenya Cane

Msanii wa Sauti Sol, Savara ametangazwa kuwa balozi mpya wa knywaji cha Kenya Cane

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Savara amesema ni jambo la faraja kufanya kazi na Kenya Cane kwani huo ni mwanzo wa ushirikiano mzuri kati yake na kampuni hiyo.

Lakini pia ameishukuru uongozi wake pamoja na wadau wote waliofanikisha dili hilo huku akiahidi kuiongezea kampuni hiyo mauzo kutokana na ushawishi kwenye jamii.

“I have worked hard to bring out my genius through art. I am on my journey to more greatness and I am proud to partner with Kenya Cane as the Official Brand Ambassador.

I appreciate all parties that made this possible. I love my team. Now to more amazing art. Twende kazi #TheGreatsToastTwice”, Ameandika Instagram

Hata hivyo Kampuni ya Kenya Cane imesema imeingia mkataba na Savara kwa kuwa wanaamini atasaidia kuzinyanyua bidhaa za kampuni hiyo kuwafikia wateja wengi.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke