Nyota wa muziki kutoka nchini Nigeria, msanii Simi anazidi kufanya vizuri kupitia mauzo ya mtandaoni ya nyimbo zake.
Simi amefanikiwa kushika rekodi ya kuwa msanii wa kike Afrika kufikisha Streams Milioni 100 kwenye platform ya kuuzia muziki ya Audiomack kwa nyimbo zake zote. Hadi sasa ana jumla ya streams Milioni 124.
Simi ambaye jina lake halisi ni Simisola Bolatito Kosoko kwa upande wa wasanii wa kike amewapiku wakali kama Tiwa Savage ambaye ana streams million 83.7M, Tems million 64.2, Yemi Alade million 24 na wengine wengi.