You are currently viewing SOULJA BOY AFUNGUKA SABABU ZA KUTOFANYA KOLABO NA TEKASHI 69

SOULJA BOY AFUNGUKA SABABU ZA KUTOFANYA KOLABO NA TEKASHI 69

Rapa kutoka Marekani Soulja Boy amefunguka na kudai kuwa hatokuja kufanya Kolabo na rapa mwenzake Tekashi 69 hadi mwisho wa dunia.

Kwenye mahojiano na Podcast ya Mtangazaji Raquel Harper “It’s Tricky with Raquel Harper”  rapa hyo aliulizwa ni namna gani atalipokea ombi la Kolabo kutoka kwa Tekashi 69 ambapo, alijibu kwa kusema kwamba  “Haiwezekani, sitakuja kufanya wimbo na wewe (6ix9ine), hatuwezi kufanya wimbo na analijua hilo, hatarajii kupata verse ya Soulja Boy, anafahamu hilo.”

Utakumbuka mwaka wa 2019 kwenye mahojiano na The Breakfast Club, Soulja Boy alisema Tekashi 69 ni zao lake kwani anaamini amemshawishi kuingia kwenye muziki ambapo aliishia kumuita mtoto wake.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke