You are currently viewing Spice Diana afunguka kuhusu bifu za wasanii

Spice Diana afunguka kuhusu bifu za wasanii

Msanii kutoka nchini Uganda Spice Diana amedai kwamba ugomvi miongoni mwa wasanii haisaidi kuwajenga kisanaa

Kwenye mahojiano yake hivi karibuni amesema wasanii wanaojihusisha na bifu kwa lengo la kutanua wigo wao kimuziki, wanaharibu brand au chapa zao  kwenye jamii.

Hitmaker huyo wa “Boss” amesema kwa sasa ana muda wa kupishana na wasanii wenzake kwani ameamua kuwekeza nguvu zake kujiboresha kisanaa kwa ajili ya kukuza brand yake.

Utakumbuka Spice Diana amekuwa akihusishwa kuwa kwenye ugomvi na wasanii Sheebah Karungi pamoja na Gravity Omutujju jambo ambalo yeye binafsi amekuwa akikanusha kwenye mahojiano mbali mbali.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke