You are currently viewing SPICE DIANA AKANUSHA KUTOALIKA WASANII KWENYE UZINDUZI WA STARGAL EP

SPICE DIANA AKANUSHA KUTOALIKA WASANII KWENYE UZINDUZI WA STARGAL EP

Msanii wa Source Management, Spice Diana amepuzilia mbali uvumi unasambaa mtandaoni kwamba hakuwaalika baadhi ya wasanii kwenye uzinduzi wa EP yake mpya Star Gal.

Katika mahojiano yake hivi karibuni amesema madai hayo hayana ukweli wowote kwa kuwa alituma mwaaliko kwa kila msanii kupitia uongozi wake.

Mkali huyo wa ngoma ya “Tujooge” amesema hana ugomvi wowote na msanii yeyote nchini uganda na kama kuna msanii hakupokea barua ya mwaaliko, uongozi wake ndio wakulaumiwa kwa kutomfikishia ujumbe.

Kauli ya Spice diana imekuja mara baada ya wasanii Gravity Omutujju na Lydia Jazmine kudai kuwa hawakupata mwaaliko wa kuhudhuria uzinduzi wa EP mpya ya Spice Diana

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke