You are currently viewing TANASHA DONNA AWATOLEA UVIVU WANABLOGU WANAOENEZA UMBEA KUHUSU MAISHA YAKE

TANASHA DONNA AWATOLEA UVIVU WANABLOGU WANAOENEZA UMBEA KUHUSU MAISHA YAKE

Staa wa muziki nchini Tanasha Donna ameonyesha kusikitishwa na jinsi habari kuhusu maisha na muziki wake inavyoripotiwa.

Kupitia waraka mrefu aliyochapisha kwenye mtandao wa Instagram Tanasha Donna amesema watu wamekuwa wakiangazia sana mabaya yake propaganda badala ya kumuunga mkono kwenye muziki wake.

Mrembo huyo amewataka wanablogu na vyombo vya habari nchini kuwatangaza wasanii wa Kenya badala ya kueneza umbea ambao hauna ukweli wowote.

Hitmaker huyo wa “Gere” ametoa changamoto kwa wa Kenya kuendelea kustream nyimbo za wasanii wao wanaowapenda kama njia ya kuwasapoti.

Kauli ya Tanasha Donna imekuja mara baada ya kudaiwa kuwa alishindwa kulipa kampuni moja inayojihusisha na masuala ya surgery shillingi laki nane za Kenya baada ya kupewa huduma ya upasuaji yaani plastic surgery kuuweka mwili wake sawa

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke