You are currently viewing TIMU YA KAMPEINI YA KANYE WEST YAKIRI KUIBIWA MAELFU YA FEDHA

TIMU YA KAMPEINI YA KANYE WEST YAKIRI KUIBIWA MAELFU YA FEDHA

Timu ya kampeni ya Kanye West imetoa madai ya kuibiwa kiasi kikubwa cha pesa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa Marekani mwaka 2020, kwa njia za ulaghai.

Kiasi cha pesa kilichoibiwa na mtu ambaye hakuwa kwenye team hiyo ya kampeni ya kanye west kimetajwa ni zaidi ya shilingi laki 4 za Kenya.

Fedha hizo zilikuwa zikiibwa kuanzia Disemba mwaka wa 2020 hadi Februari mwaka wa 2021 katika akaunti ya Kanye West iliyopo katika First Bank of  Wyoming.

Kanye West ambaye alikuwa akiwania kiti cha urais katika uchaguzi mkuu mwaka wa 2020  nchini Marekani alishindwa lakini hivi karibuni kwenye moja ya mahojiano yake ameahidi kuwania tena kiti hicho cha urais mwaka wa 2024.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke