You are currently viewing WASANII WA KENYA WAPOKEA MIRABAHA YAO KUTOKA PRISK

WASANII WA KENYA WAPOKEA MIRABAHA YAO KUTOKA PRISK

Wanamuziki wa Kenya wamepokea mirabaha yao kutoka kwa Chama cha Haki ya watumbuizaji nchini PRISK, iliyopewa mamlaka na bodi ya hakimiliki nchini KCB kuwasimamia kazi za wabunifu wote wanaojihusisha na sanaa.

Kila msanii aliyesajiliwa na PRISK amepokea shillingi 1,215 za kenya kama mapato yake jambo ambalo baadhi ya wasanii wameonekana kupokea shingo upande wakisema kwamba pesa hiyo ni kidogo sana ikilinganishwa na namna muziki unatumika maeneo ya umma na mengine ya burudani.

Mapema mwezi huu Rais Uhuru Kenyatta alitia saini msaada wa marekebisho ya hakimiliki kuwa sheria mpya ambayo inatoa mwongozo ya jinsi wabunifu au wasanii wanapaswa kupokea mgao wa mapato ya kazi zao isiyopungua asilimia 52.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke