Mwigizaji kutoka Marekani Will Smith ameripotiwa kuwa yupo kituo cha kupokea matibabu ya Kisaikolojia (Rehab).
Tovuti ya Hollywood Insiders imeliambia gazeti la The Sun kwamba mwigizaji huyo amefika kwenye kituo hicho na atakuwa akipatiwa msaada namna ya kupambana na msongo wa mawazo.
“He will be getting help on dealing with stress… this is unquestionably the battle of his career” – chanzo cha karibu na Smith kimeliambia The Sun.
Haya yanajiri ikiwa ni wiki chache zimepita kufuatia tukio la kumchapa kibao jukwaani mchekeshaji Chris Rock kwenye hafla ya Tuzo za Oscars, 2022.