You are currently viewing ZIZA BAFANA AMCHANA BEBE COOL KISA ORODHA YAKE YA WASANII WALIOFANYA VIZURI MWAKA 2021

ZIZA BAFANA AMCHANA BEBE COOL KISA ORODHA YAKE YA WASANII WALIOFANYA VIZURI MWAKA 2021

Mwanamuziki anayesuasua kimuziki nchini Uganda Ziza Bafana hana furaha kabisa baada ya kutoonekana kwenye orodha ya wasanii wa kila mwaka ambayo hutolewa na msanii mwenzake Bebe Cool.

Bafana, ambaye alifanya vizuri mwaka wa 2021 kwa kuachia magoma makali anadai kuwa Bebe Cool alipoteza mweelekeo katika tasnia ya muziki nchini Uganda kwani siku hizi hajakuwa akiachia muziki mzuri kama kipindi cha nyuma.

Hitmaker huyo wa “Embuzi” amesema Bebe Cool,anatumia orodha yake ya kila mwaka ya wasanii waliofanya vizuri kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwenye vyombo vya habari nchini Uganda.

Ikumbukwe Bebe Cool hajawahi kuwa na uhusiano mzuri na mwanamuziki mwenzake Ziza Bafana baada ya msanii huyo kuanza kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya miaka kadhaa iliyopita.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke