You are currently viewing Zuchu atangaza kufanya ziara ya muziki nchini Marekani

Zuchu atangaza kufanya ziara ya muziki nchini Marekani

Msanii wa Bongofleva, Zuchu anatarajia kufanya ziara yake kimuziki (tour) nchini Marekani kuanzia Novemba 18 hadi Desemba 3 mwaka huu.

Ziara hiyo ya Zuchu ni pamoja na kutumbuiza kwenye hafla ya utoaji wa tuzo za African Muzik Magazine Awards (AFRIMMA) zitakazotolewa Novemba 19 huko Dallas, Texas nchini Marekani ambapo Zuchu anawania kipengele cha Msanii Bora Afrika.

Hii itakuwa ni ziara ya kwanza ya Zuchu nchini Marekani tangu ajiunge na WCB Wasafi Aprili mwaka 2020, hivyo anajiunga na Staa mwingine wa Bongofleva, Ali kiba ambaye tayari yupo nchini humo kwa ajili ya tour yake.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke