You are currently viewing ZULITUMS ATOA CHANGAMOTO KWA WASANII WA UGANDA KUTUMIA KIINGEREZA KWENYE NYIMBO ZAO

ZULITUMS ATOA CHANGAMOTO KWA WASANII WA UGANDA KUTUMIA KIINGEREZA KWENYE NYIMBO ZAO

Mwanamuziki kutoka nchini uganda Zulitums ametoa changamoto kwa wasanii nchini humo kuanza kutumia lugha ya kiingereza kwenye nyimbo zao ili muziki wa uganda uweze kufika mbali zaidi.

Zulitums amesema licha ya wasanii wa uganda kutoa muziki mzuri wengi wao wamekuwa wakitumia lugha ya luganda kwenye nyimbo zao jambo analosema limewafanya wasanii kushindwa kutanua wigo wa muziki wao kwenye nchini zingine.

Zulitums ni mmoja wa wasanii nchini uganda walioshindwa kuupeleka muziki wao kimataifa hadi pale alipojiunga na lebo ya muziki ya Black Avie iliyoko nchini Nigeria ambayo imebadilisha aina ya muziki wake.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke